
TUNDA: Yeye kama ameamua kujitoa Tip Top, inabidi aachane na ngoma hiyo, kwakuwa mimi ndiye mtunzi, nilimpa shavu tu ili kumuweka juu kwakuwa kipindi hicho hakuwa akisikika. Hiyo ishu ya kujitoa inatufanya sisi wasanii wa familia hiyo tuonekane hatuna msimamo.
SPARK: Kweli yeye ndiye alikuja na idea ya wimbo huo lakini bila mimi, ngoma ya Nipe Ripoti isingekuwa vile. Mimi ndiye niliyeandika vesi yangu pamoja na korasi ambayo niliifanyia studio kwa MJ, shahidi wangu Marco Chali. Au kama Tunda anabisha uwekwe mpambano wa kuimba ngoma hiyo ili tuona nani atapotezwa. Mimi nimejitoa Tip Top kwa maslahi yangu, yeye pia inabidi ajizungumzie yeye na siyo kunitaja mimi kwenye intavyuu anazofanya.
Friday, August 21, 2009
Posted in | |
0 Comments »
One Responses to "EXCLUSIVE: TUNDA, SPARK WAPIGANA BIT"