Z-Anto n Madee baada ya shoo

Kijana aliyepata kufanya vyema kunako game ya muziki wa kizazi kipya, Z-Anto juzi kati alionesha dalili za kurudi ndani ya kundi lililomtoa, Tip Top Connection baada ya kudandia stejini na kusapoti uzinduzi wa kundi hilo uliyopigwa ndani ya Club Sun Nsirro iliyopo pande za Sinza, Dar.
Ilikuwa kama 'sapraizi' wakati MC wa shughuli hiyo, Mwalubadu alipomtaja Z-Anto kuwa anapanda stejini na kusapoti uzinduzi huo, wengi hawakuamini kwakuwa 'dogo' aliondoka kundini kwa jazaba huku akianika madai yake kwa viongozi wa Tip Top kunako vyombo kadhaa vya habari.
Alipopanda jukwaani aliwakumbusha mashabiki wake kwa ngoma ya Binti kiziwi kabla ya kumalizia na hii inayotamba hivi sasa ikiwa na jina la 'Kisima cha malovedavi'. Baada ya tukio hilo ebwanadaah ilimtafuta memba wa kundi hilo, Madee na kumuuliza inakuwaje mchizi karudi kundini kimya kimya? "Anto bado hajarudi kundini, lakini tupo katika maongezi, inawezekana tukawa naye tena pamoja," alijibu.
Wengine waliokuwepo kwenye uzinduzi huo na kutoa sapoti ya kutosha ni hawa hapa chini.

Kabla ya kupanda steji Linah aliweka tumbo fresh



Mwasiti naye alifanya vivyo hivyo ili kuongeza nguvu


Dj Choka na Lulu pia walikuwepo

Kassim baada ya shoo

Young Dee alisapoti

Mfalme wa Sala Sala, Goldzilla alionesha kiwango

Mimi pia (wa pilia kushoto) niliwakilisha na wana. Thanks Dj Choka kutugonga picha hii
Sunday, September 12, 2010
Posted in | |
0 Comments »
One Responses to "Z-ANTO ARUDI STEJINI TIP TOP"