ILI MUZIKI WETU UWEZE KWENDA KIMATAIFA NI LAZIMA TUBADILIKE, SAPOTI YAKO PIA MUHIMU

Benja katika pozi tofauti


Kutoka ndani ya Kundi la mambo Jambo, kijana Benjamini Busungwi a.k.a Benja wa Mambo Jambo katoka tena kivyake, hivi sasa akiwa amesimama na AT wa 'Nipigie' katika ngoma yake mpya yenye jina la 'Nimefulia'.
Akipiga stori na ebwanadaah Benja alisema kwamba, ngoma imefanyika Mzuka Records, pandeza Bahari Beach, Dar essalaam. Ni kazi ambayo ameigonga kivingine ndiyo maana iko juu ile mbaya.

Read More......
Saturday, January 30, 2010 Posted in | | 0 Comments »












Hizi ni baadhi ya picha zinazopatikana ndani ya video ya ngoma ya Mambo Bado ya kwake Chegge featureling Lady Jaydee.





Nani asiyefahamu kwamba mtoto wa Mama Said, Chegge Chigunda kutoka Kiumeni hivi sasa yuko hewani na ngoma mpya? Naweza kusema mwaka huu umeanza poa kwake kwaku kazi hiyo yenye jina la Mambo Bado iliyompa shavu Lady Jaydee inakimbiza mbaya kunako luninga na redio. Big Kijana kwa kazi nzuri.




Read More......
Posted in | | 0 Comments »

Hapa nikimkaribisha aliponitembelea ofisini
Zay B akionesha bado yuko gado

Hii ndiyo ndinga yake

Huu ndiyo mjengo wake

Kutoka Bongo mwana Hip Hop wa kike aliyeleta mapinduzi katika game ya muziki wa kizazi kipya kwa upande wa wasichana, Zainabu Lipangile a.k.a Zay B mwishoni mwa wiki iliyopita alidondoka ndani ya blog hii na kupiga stori mbili tatu ikiwemo kutangaza baadhi ya aseti anazomiliki hivi sasa kama alivyofanya Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda.

Zay B alisema kwamba wapo baadhi ya watu wakiwemo wasanii wenzie wamekuwa wakivumisha maneno mitaani kwamba hivi sasa amefulia baada ya kupotea kwenye game kwa muda mrefu kitu ambacho amekikanusha, ndiyo sababu iliyomfanya atangaze mali zake.

“Unajua watu wengine huwa wanakosa ishu za kuongea, mimi kutosikika siyo kwamba nimefulia, kuna ishu kibao nafanya zinazoniingizia kipato, kwanza muziki wa Bongo haulipi na umejaa majungu. Ningekuwa nimefulia ningeweza kujenga nyumba au kununua gari?” Alihoji Zay B huku akionesha picha za nyumba yake zilizokuwa kwenye simu.

Mwanadada huyo alisema kwamba mjengo huo ameushusha pande za Buyuni, Pugu nje kidogo ya Dar es Salaam huku akimiliki gari aina ya Toyota Premio. “Mbali na hayo pia nimesaini mkataba wa kufanya kazi ya muziki na Kampuni ya Butile Africa Group ya Afrika Kusini, watu wasifikiri nipo nipo tu, sijafulia kihiivyo,”.


Read More......
Tuesday, January 19, 2010 Posted in | | 0 Comments »

Hatimaye kipindi cha likizo kwa madenti wengi kimemalizika na kinachofuata ni wazazi kuumiza vichwa watoto wao watarudije shule wakati sikukuu zimekata mkwanja wote. Mimi namshukuru God kwa kuniwezesha kumpiga pamba za school kid wangu na kulipa ada za hapa na pale. Masomo mema my baby, Brian endelea kukaza buti class.

Read More......
Sunday, January 10, 2010 Posted in | | 0 Comments »


Sugu na Stara stejini siku ya uzinduzi

Albamu mpya ya mwana Hip Hop ‘bei mbaya’ Bongo, Joseph Mbilinyi ‘Mr. II’ inayokwenda kwa jina la Veto, tayari imeanza kukubalika, kitaani kutokana na idadi kubwa ya Wamachinga kutoa ripoti chanya kuhusu mauzo.

Akipiga stori na ebwanadaah juzi Sugu alisema kwamba, Wamachinga walioripoti kwake katikati ya wiki iliyopita walisema kuwa jinsi wanavyosumbuliwa mtaani na wadau wa burudani wanaoiulizia Veto, ni wazi kwamba inakubalika, hivyo wengi wanapenda kuipata.

Sugu alisema kuwa ameona Wadosi ambao walikuwa wanauza zamani ni wazinguaji, hivyo ameamua kubadilisha upepo kwa kuuza mwenyewe, akiwatumia Wamachinga nchi nzima ili kupata fedha yenye maelezo halisi.

“Watu wananipigia simu, wananiuliza Veto vipi? Wadosi wanatuumiza, kwahiyo tunasambaza na Wamachinga, kwahiyo popote pale mdau akimuona Mmachinga amwite amuulize Veto, atapata albamu bora ya Hip Hop,” alisema Sugu.


Read More......
Posted in | | 0 Comments »


Tulianzia Shoprite, kununua vitu viwili vitatu
Kisha tukawasili katika fukwe za Coco Beach
Kilichofuata ni full kuogelea


Washikaji zangu wengi wa karibu wametaka kufahamu siku ya mwaka mpya nilikuwa wapi, kiukweli mimi nilikuwa bize zaidi na familia.

Read More......
Tuesday, January 5, 2010 Posted in | | 0 Comments »