ILI MUZIKI WETU UWEZE KWENDA KIMATAIFA NI LAZIMA TUBADILIKE, SAPOTI YAKO PIA MUHIMU

Ishu mpya iliyodondoka pande hizi za ebwanadaah kutoka kwa Rais wa Manzese a.k.a Madee ambaye bado yupo kwenye majonzi ya kutosha kufuatia kifo cha mpenzi wake, inasema kwamba hivi sasa jamaa ameamua kutulia na kuandika kitabu kitakachoweka wazi mambo yake kibao likiwemo hilo la msiba.

“Mimi na Pendo tulipanga mambo mengi, aliwahi kuniambia malengo yake ni kusoma zaidi na baadaye kuwa mlezi wa watoto yatima. Lakini zaidi nitayaweka kwenye kitabu changu ambacho pia kitakuwa na full stori ya maisha niliyopitia mpaka nilipofika leo,” alisema.


Read More......
Sunday, March 21, 2010 Posted in | | 0 Comments »

Master J akicheki ninavyowajibika kuandaa moja ya page za burudani

Muda mwingi alionesha kufurahishwa na kazi niliyokuwa naifanya

Baada ya ziara hiyo niliagana na Master J


Siku moja iliyopita nilipata zali la kutembelewa na Prodyuza galacha in Bongo Music, Joachim Kimaryo ‘Master J’ na kufanya naye interview katika maeneo kadhaa muhimu. Akiwa ofisini kwetu, Sinza, Bamaga, Dar es salaam mchizi alipata fulsa ya kujionea jinsi tunavyoandaa magazeti yetu mpaka yanawafikia wasomaji. Jay ambaye ni mmoja wa Maprodyuza walioishep Bongo Fleva wakati inasimama na kukubalika pamoja na aina nyingine ya muziki, alizungumzia mambo yafuatayo.

Mosi, alielezea BSS, pili ni kuhusu Bongo Fleva ilipotoka na inapokuja na tatu ni yanayohusu studio yake, lebo na wasanii anaowasimamia kwa jumla.

Kuhusu BSS, Jay alisema kwamaba, washindi wa taji hilo linaloheshimika kwa Watanzania hivi sasa, hawaoneshi cheche sokoni kwa sababu hawawezi kuandika.

Anasema: “Tatizo si BSS, Benchmark, Madam Rita wala majaji, tatizo ni wasanii wenyewe kwa sababu hawana uwezo wa kuandika na kuandaa nyimbo zao ili zikubalike.

“Wasanii wanaposhiriki BSS, wanaimba nyimbo za watu, kwahiyo wanaonesha uwezo wao kwa kuimba tu, hivyo wanakubalika na wanapigiwa kura lakini kwenye kutunga hakuna.

“Hii ndiyo sababu Jumanne Idd (mshindi mwaka 2007), Misoji Nkwabi (2008) wameishia njiani, unaona hata Pascal Cassian (2009) bado hajasimama, angalau Peter Msechu (1st runner up 2009) anaokoa jahazi.

“Nilitoa ofa ya wasanii wote walioingia Top 5 kurekodi nyimbo kwenye studio yangu (MJ Production) ili kuonesha mwanga ili Watanzania waone kwamba kumbe inawezekana Staa wa BSS akawa mfanyabiashara mzuri wa muziki nchini.

“Hilo tumeliangalia kwa mapana na mikakati ya BSS mwaka huu ni pamoja na kutafuta watu watakaowaandikia nyimbo washindi na kuwachagulia ala, kwahiyo baada ya shindano wataingia studio na kufyatua mawe yenye akili”. Mengi zaidi endelea kuchungulia blog hii.

Read More......
Posted in | | 0 Comments »

Mimi na Ambwene Yesaya 'A.Y' tukiwa katika pozi

Kutoka pande za Sinza, Dar es Salaam, Mzee wa Commecial, Ambwene Yesaya a.k.a A.Y amesema na ebwanadaah kwamba, mwaka huu wa 2010 kwake utakuwa ni vita coz amejipoanga kuachia jiwe juu ya jiwe ili kwenda kimataifa zaidi kama alivyoanza na Bed & Breakfast na Queens & Kings.

Read More......
Saturday, March 20, 2010 Posted in | | 0 Comments »

ShowBiz ambayo iko juu kukuletea wewe msomaji michongo inayoendelea kwenye game ya burudani, leo imeidaka ishu mpya kutoka kwa Mike Mwakatundu a.k.a Mnyalu ambaye kitambo kirefu alipotea kwenye mradi wa muziki.

Akiwa ni mwajiriwa wa kampuni moja ya simu za mkononi Bongo, Mnyalu amerudi kivingine akisikika na ngoma yenye jina la I Love U, huku uvumi ukiwa umeenea kitaani kwamba alipotea kwenye sanaa coz alikuwa bize akimsaidia waifu wake kumlea mtoto wao, Mike Junior (pichani).


Read More......
Posted in | | 0 Comments »

Aliyekuwa mchumba wa msanii, Madee aliyefariki dunia juzi kwa ajali ya basi, Pendo anatarajiwa kuagwa Jumatatu Machi 15, 2010 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kuanzia saa 4 asubuhi hadi 6 kabla ya kusafirishwa kuelekea Moshi kwa mazishi. Mungu aiweke Roho ya Marehemu Mahali pema, peponi.

Read More......
Sunday, March 14, 2010 Posted in | | 0 Comments »


Ishu mpya iliyodondoka pande hizi inawahusu mastaa wawili wenye majina in the Bongo Flava, Khamis Mwinjuma ‘FA’ na Ambwene Yesaya ‘A.Y’, wako hand in hand katika kusukuma gurudumu la maisha.

Akipiga story na ebwanadaah juzikati, FA alitoa bonge la surprise pale alipoweka plain kwamba, kwa sasa meneja wake ni A.Y ambaye yuko mbioni kumaliza masomo yake ya biashara yaliyokuwa yakimuweka tight.

Akiwa na three weeks only tangu arejee Bongoland from kiwanja, mtu mzima FA alisema na safu hii kuwa mapema next week ataanza project mpya na meneja wake ambayo wataipa title hapo baadaye.

“Project hiyo itafanyika ndani ya B-Hits Company chini ya maprodyuza Hermy B na Pancho,” alisema.


Read More......
Posted in | | 0 Comments »

Unamkumbuka yule dogo aliyeibuliwa na King Crazy GK na kutamba ndani ya kundi la East Coast Team? Anaitwa Jumaa aliyesimama vyema kwenye ngoma kama 'Komaa nao' na 'Piga Manati'. Baada ya umoja huo kusambaratika na yeye kupotea kwenye game kwa muda mrefu, sasa anarudi tena. Endelea kucheki na blog hii iili ufahamu dogo anarudi vipi.

Read More......
Posted in | | 0 Comments »

Mimi na wafanyakazi wenzangu, Walter a.k.a Mcharuko (katikati) na Cralence a.k.a Mwalumwalu tukijipongeza kwa juisi baada ya kazi ngumu ya kutwa nzima (huwa tunaita kufuta mafolda yenye virus yaliyojaa vichwani). Ilikuwa ni tafrija fupi iliyoandaliwa na MD wetu, Eric Shigongo, ndani ya Hotel ya Atriums, liyopo Sinza, hivi karibuni.

Read More......
Posted in | | 0 Comments »

Madee na Pendo enzi za furaha yao
Huzuni imechukua nafasi yake

Taarifa ya huzuni iliyodondoka ndani ya ebwanadaah hivi punde inasema kwamba, msanii Hamad Ally a.k.a Madee kutoka ndani ya familia ya Tip Top Connection amefiwa na mpenzi wake wa siku nyingi,Pendo.
Akiongea na mtandao huu kwa njia ya simu leo asubuhi,Madee alisema kwamba Pendo amefariki dunia jana kwa ajali ya basi la Shabiby linalofanya safari zake kati ya Dar es Salaam na Dodoma iliyotokea jana. Mimi kama mmoja wa ndugu wa karibu na msanii Madee natoa pole nyingi, namuomba awe mvumilivu katika kipindi hiki kigumu.
Mungu alitoa na Mungu ametwaa.


Read More......
Thursday, March 11, 2010 Posted in | | 0 Comments »

Hapa nikipeana mkono na Mbangu huku 'mkubwa' Sifael (katikati) akishuhudia
Stori ziliendelea. Fancis (wa pili kutoka kulia) akichungulia kwa mbali

Siku chache baada ya kuachiwa huru kutoka katika kifungo cha maisha, watoto wawili wa mwanamuziki Nguza Viking 'Babu Seya', Nguza Mbangu na Francis walitutembelea ofisini, mi pia nilipiga nao stori mbili tatu tukabadilishana mawazo.

Read More......
Monday, March 1, 2010 Posted in | | 0 Comments »

Staa wa Bongo Flava, Zainab Lipangile ‘Zay B’ ameibuka na kuweka plain kwamba, lile bifu liliwahi kugonga vichwa kati yake na mwanamuziki mwenzake, Happy Thadei ‘Sister P’ bado liko pale baada ya kuwepo evidence kuwa still hawaivi in the same pot.
Akipiga stori na safu hii, jijini Dar mwishoni mwa wiki iliyopita, Zay B alidai kwamba hawezi kuwa in a good understanding na Sister P pamoja na kwamba walishajaribu kuwa close, lakini wakaja kuhitilafiana tena na sasa uhusiano wao ni sifuri.
“Sitomsamehe Sister P milele kwa vitendo alivyonifanyia, hivi sasa anajifanya hana bifu na mimi lakini inawezekana moyoni mwake hayuko hivyo. Hivi sasa akifanya intavyuu na baadhi ya vyombo vya habari anawaambia yupo katika mishemishe za kurekodi na mimi na kwamba tumeshakutana tukaongea, kitu ambacho siyo kweli, hata akija na Rais Obama siwezi kufanya naye kazi,” alisema Zay B ambaye alitambulishwa na ngoma yake yenye jina la Gado, kabla Sister P hajatoka na ‘Anakuja’ kunako miaka ya 2002.
Zay B na Sister ni wasanii wa kike wa long time katika Tasnia ya Bongo Flava ambao some years huko nyuma waliwahi kuwa na bifu kali na kauli ya Zay B inayotoa tafsiri kuwa bado mtiti uko palepale. Safu hii itaendelea kucheki na Sister P ili kujua kama bado ndoto zake za kurekodi na Zay B ziko pale pale.

Read More......
Posted in | | 0 Comments »

Ze Dudu

The long time Artist wa Bongo Flava, Godfrey Tumaini a.k.a Dudubaya’, ambaye hivi sasa anasimama vema na ngoma mpya yenye jina la Push Push juzikati alipiga stori na Abby Cool & MC George over the weekend na kuchana kwamba, machungu aliyonayo moyoni hivi sasa yanamfanya asikie kichefuchefu pale msanii chipukizi anapomuibukia kumuomba msaada.
Mchizi alisema kuwa, machungu hayo yanatokana na fadhila ‘mbovu’ anazozipata kutoka kwa baadhi ya mastaa wa muziki wa kizazi kipya ambao alijitahidi kuwasapoti mpaka wakatoka lakini mwisho wa siku wakaamua kumdis bila sababu.
“Hivi sasa nina machungu sana, kiasi kwamba ‘andagraundi’ akija kuniomba msaada nasikia kichefuchefu kwasababu mwisho wa siku wanakosa shukrani kama ilivyokuwa kwa Hamidu ambaye nilimkuta yuko darasa la pili lakini shule haendi kutokana na matatizo ya familia yake, nikajitahidi kumsomesha mpaka akamaliza darasa la saba, lakini mwisho wa siku nikaonekana sina maana kwake”, alisema Ze Dudu.
Mastaa wengine aliowataja kuwasapoti mpaka wakachomoka kwenye game ni pamoja na Afande Sele ‘Baba Tunda’ msanii wa kike, ‘Besta’, Sister P, Pig Black na Crew ya Mabaga Fresh ambayo aliisaidia kutengeneza ngoma yao ya kwanza, ‘Mtulize’ kabla hawajachukuliwa na P-Funk na kugonga Mtulize remix wakiwa na Nature.

Read More......
Posted in | | 0 Comments »

Cheki pozi jipya la Misosi
Juacali: Niaje watu ya nyerereeeee!

Artist wa Bongo Flava, Joseph Rushau a.k.a Bwana Misosi, ameibukia pande za Tanga na kusema na safu hii kwa njia ya simu kwamba alikuwa tight na mambo ya kifamilia, ili kuvunja ukimya huo, soon atadondosha ngoma moja funiko inayokwenda kwa jina la Huwezijua ambayo amempa shavu Juacali kutoka Kenya.
Akipiga stori na Abby Cool & MC George Over Da Weekendi juzikati, Misosi aliyethubutu ku-shine na songi la Nitoke Vipi na baadaye Mabinti wa Kitanga, alisema kuwa ngoma hiyo aliyomshirikisha mchizi kutoka kwa Mwaikibaki, imefanyika hapa Bongo katika Studio ya Fish Crab iliyopo maeneo ya Jangwani, jijini Dar ukiwa ni mkono wa prodyuza yanki, Lamar.

Read More......
Posted in | | 0 Comments »