ILI MUZIKI WETU UWEZE KWENDA KIMATAIFA NI LAZIMA TUBADILIKE, SAPOTI YAKO PIA MUHIMU

Hapa tukisabahiana, kanizidi urefu kidogo tu, siyo sana
Leo asubuhi staa wa basketball kule kwa Obama na duniani kwa ujumla, Hasheem Thabeet Manka aliibuka ofisini kwetu kwa ajili ya kutupa Hi na shukrani za pekee kwa sapoti tuliyompa na tunayoendelea kumpa hadi kufikia hapo alipo hii leo. Mimi pia nilipiga naye stori mbili tatu tukakumbushana enzi zile alipokuwa anapiga shoo za Bongo Flava. Tumetoka mbali jamani.

Read More......
Friday, April 23, 2010 Posted in | | 0 Comments »

Hapa A.Y (kushoto) akikabidhiwa tuzo

Artists wawili wa Muziki wa Kizazi Kipya wenye heshima tele Bongo, Ambwene Yesaya, A.Y na Lawrence Malima Madole a.k.a Marlow, wamekomba tuzo za TEENEZ zilizotolewa pande za Nairobi, Kenya. Aprili 17, mwaka huu.

Story iliyotua kunako blog hii imeweka kweupe kwamba, ishu hiyo ambayo kwa hapa Bongo imekuwa kama ‘sapraizi’ kwakutokuwa na promo ya kutosha ilichukua nafasi pande hizo weekend iliyopita ambapo A.Y aliibuka na ‘awadi’ ya Msanii Bora wa Afrika Mashariki.

Kwa upande wa Marlaw aliondoka na tuzo ya the most downloaded song kupitia ngoma yake ya Pipi.

“Kwangu mimi ni heshima inayoendelea kuwepo, inanipa moyo ili niongeze bidii katika kuandika ngoma kali,” alisema A.Y mbele ya ebwanadaah.


BEST EAST AFRICAN ARTIS CATEGORY:


MARLAW-TANZANIA

WEASEL AND RADIO-UGANDA

AY-TANZANIA

BLU 3-UGANDA


Read More......
Posted in | | 0 Comments »

J. Martins alipodondoka Bongo
Hapa akishoo lavu na A.Y (kushoto) pamoja na mdau (katikati)
J Martins stejini

Baadhi ya wafanyakazi wa Zain na wageni waalikwa wakitoa sapoti kwa mchizi

Mchizi kutoka pande za Nigeria, J. Martins anayeendelea kufanya maajabu kunako game ya muziki kupitia ngoma zake kadhaa ikiwemo Iva jana usiku alimaliza kazi iliyomleta Bongo kwa kuangusha burudani ya ukweli ndani ya ukumbi uliyopo kwenye mjengo mpya wa Kampuni ya simu za mkononi ya Zain uliyopo mitaa ya Moroko, Dar.

Read More......
Tuesday, April 20, 2010 Posted in | | 0 Comments »

Jana jioni mwanadada Zainabu Lipangile a.k.a Zay B alinitumia ujumbe mfupi wa maandishi (SMS) akionesha kuguswa na tuzo za muziki, Kili 2009-2010. Nami naudondosha kwenu kama ifuatavyo yakiwa ni maoni yake.
"Kili Music Awards kwanini wasanii wa kike tunaofanya muziki wa Hip Hop hawatupi nafasi ya kushiriki? Kila mwaka wanatutenga, category zote ziko wanawake na wanaume kasoro Hip Hop.
Unajua tuzo ni heshima na silazima apewe Zay B ila tufikiriwe, suala la kusema wasanii wa kike wachache si kweli, tuko zaidi ya watano ambao ni maarufu, siyo kwangu ishu kupewa tuzo, ila acheni ubaguzi. Mimi ni Mama Afrika mtetezi wa wanawake, tupeni haki yetu".

Read More......
Sunday, April 18, 2010 Posted in | | 0 Comments »

Kama wewe pia unainjoi kuangalia muvi za komedi kama mimi ni lazima utakuwa umeshaicheki Scooby Doo. Nimevutiwa na picha hii nikaamua kuidondosha hapa.

Read More......
Friday, April 16, 2010 Posted in | | 0 Comments »

Mkoloni, Ze Dudu na Afande Sele

The Bongo Hip Hop Legend, Godfrey Tumaini ‘Dudubaya’ amezindua harakati mpya ya kuitetea Hip Hop na Bongo Flava pamoja na wasanii wake kwa kutoa CD inayoelezea kinagaubaga unyonyaji unaoendelea aliyoipa jina la Nguruwe. In that CD, Ze Dudu a.k.a Baba Willy anawachana presenters & DJ’s ambao wanatajwa kuishi kimjini mjini kwa mgongo wa wasanii ambao wanawanyonya.

Mbali na kuwadisi presenters & DJ’s hao, pia Dudu ametoa shut out kwa waandishi na wadau wa burudani Bongo wanaheshimu taaluma kwa kutokuendekeza rushwa.

Kwa sauti kavu, pia Dudu amewagonga nyundo baadhi ya wana Hip Hop wanaojiita wanaharakati kwamba sifa hiyo haiendani nao kwa sababu ni wanyonge na hawajui kutetea haki zao na za muziki huo kwa ujumla.

“Kuna Ma-DJ wamegoma kupiga nyimbo zangu tangu mwaka 2006, miaka minne bado nipo. Sijaenda kuomba msamaha na ninaishi, sisi ndiyo ma-legendary wa huu muziki, tumetoka nao mbali halafu watu wanakuja kula kiulaini.

“Mtu unaimba Hip Hop unajiita mwanaharakati, siku mbili nyimbo zako hazichezwi redioni unakwenda kuomba msamaha, unapiga magoti,” Ze Dudu anasikika akigonga sauti ndani ya CD hiyo.

Akichambua umafia wa baadhi ya watangazaji na Ma-DJ Bongo, Ze Dudu anamwaga kuwa kuna watu wameweka mkakati kwamba bila shilingi 500,000 hawaruhusu kupiga nyimbo redioni kitu ambacho ni sawa na unyonyaji.

“Hizo laki tano tano msanii atatoa kwa redio ngapi? Kwa uwezo upi? Halafu unatengeneza albamu kwa milioni 4, unakwenda kwa mdosi unalipwa milioni 2, msanii atapata nini?” Anahoji Ze Dudu na kuongeza:

“Mtangazaji anakupigia simu anakuuliza upo wapi? Unamjibu upo baa, baada ya dakika chache anakuja na wapambe, demu wake, wanaagiza vinywaji vya bei mbaya eti ‘bili’ yote juu yako msanii. Watu tuna familia, mimi mwanangu Willy anasoma International School.”

"Baada ya stori hiyo yenye jina la Nguruwe pati one, inakuja pati two yake ambayo naifanya na vichwa kama Mkoloni wa Wagosi wa Kaya na Afande Sele, tunataka kuwaambia ukweli wale wanaotaka kujinufaisha kupitia migongo yetu," alisema Dudu alipoongea na ebwanadaah..


Read More......
Posted in | | 0 Comments »

Baada ya kufanya vyema na kazi yenye jina la Nipe ripoti akiwa na Spark, Tundaman kutoka ndani ya familia ya Tip Top Connection amesimama tena na ngoma mpya yenye jina la Hali yangu mbaya akiwashirikisha Madee na Chegge wa Kiumeni. Ebwanadah inakupa shavu la kutosha kijana kwa kuendelea kukaza kunako game hiyo.

Read More......
Posted in | | 0 Comments »


Kutoka pande za Arusha msanii wa mzuiki wa Injili, Steven Wambura 'Pastor Wambura' ametoka tena, hivi sasa akiwa na kazi yenye jina la Roho ya Bwana.
"Wimbo huu ndiyo utabeba jina la albamu yangu mpya ambayo tayari imekamilika ikiwa na jumla ya nyimbo nane," alisema Wambura alipoongea na ebwanadah juzi kati.
Albamu ya kwanza ya Wambura ilitoka mwaka jana ikiwa na jina la Bwana ndiye Bwana, wimbo ambao ulifanya vizuri na kumtambulisha vyema katika sanaa hiyo.

Read More......
Posted in | | 0 Comments »