ILI MUZIKI WETU UWEZE KWENDA KIMATAIFA NI LAZIMA TUBADILIKE, SAPOTI YAKO PIA MUHIMU

Mlezi wa Za Big Level, Aneth (kushoto) akiwa na Best Werema

Nikisalimiana na Best Werema, muasisi wa Za Big Level
...hapa nikisalimiana na Aneth
...zikafuatia picha za pozi

Leo mchana nilibahatika kutembelewa na memba wawili wanaounda familiy ya Za Big Level kutoka Tarime mkoani Mara, Best Werema ambaye ni muasisi wa umoja huo na Aneth Kubih 'First Lady' ambaye pia ni mlezi wa chama hilo ambao nilikuwa nikiwasiliana nao kupitia mtandao kwa muda mrefu bila kuonana hasa baada ya kuvutiwa na kazi zangu ukiwemo wimbo wangu mpya, Hadithi. Vijana hawa kwasasa wapo Dar kwa ajili ya kuangalia ni jinsi gani wanaweza kuusongesha zaidi umoja wao huo kwa kuongeza idadi ya wanachama ikiwezekana nchi nzima.
"Za Big Level ni family ambayo inawahusu vijana wengi hasa wenye vipaji tofauti kwa ajili ya kusaidiana na kuhakikisha kila mmoja anafanikiwa kupitia kipaji chake, ndiyo maana kauli mbiu yetu inasomeka kwamba, 'ZA BIG LEVEL KWA VIPAJI ZAIDI'. Kama wewe ni kijana na unahisi una kipaji chochote unakaribishwa kujiunga nasi," alisema Werema. Mengi zaidi kuhusu vijana hawa tembelea tovuti yao www.zabiglevel.blogspot.com.

Read More......
Sunday, January 30, 2011 Posted in | | 0 Comments »


Baba mzazi wa msanii Joseph Gabriel Rushau 'Bw. Misosi', Gariel Rushahu aliyefariki dunia usiku wa kuamkia jana kwenye Hospitali ya Regency, Dar anatajia kuzikwa kesho Jumamosi kwenye makaburi yaliyopo maeneo ya Kinyerezi Kibaga ambako ndiko uliko msiba.
Akipiga stori na ebwanadaah jana, Misosi alisema kwamba kila kitu kuhusu mazishi kimeshakamilika kinachosubiriwa ni baadhi ya ndugu ambao wanatarajia kuwasili leo. MUNGU AIWEKE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI. AMINA

Read More......
Thursday, January 27, 2011 Posted in | | 0 Comments »

"Sisi ni FBG, wana Hip Hop toka Chuga Chuga (Arusha) tunafungua mwaka 2011 na concious joint kuelezea hali halisi ya taifa le2 na maisha ya mtaa yanavotupelekesha huku viongozi wanafuja fedha za mlipa kodi. Ngoma yetu mpya inakwenda kwa jina la 'Inaniuma kwa roho', imerekodiwa pande za Noizmekah S2dio Arachuga na harakati za kushoot video yake zinaendelea. Pia tunamalizia tape yetu tutakayoitoa "FREE" ambayo itakwenda kwa jina la "codemixxing", collection hiyo itajumuisha pia wimbo huu na nyingine kibao, kuanzia mwezi wa tatu mwaka huu mashabiki wategemee vibe za kumwaga".

Read More......
Tuesday, January 25, 2011 Posted in | | 0 Comments »

"Tuna furaha sana kwa wewe kama mdau wetu kuusoma na kuufanyia kazi wimbo wetu mpya unaokwenda kwa jina la 'Mazingira yetu'. Huu ni mmoja kati ya nyimbo ambazo zinakamilisha mipango yetu na kuifanya TMK MAJITA kuwa katika msimamo na kuzidi kusonga mbele. Kama una maoni au ushahuri unaweza kutucheki kwa namba +255767 685 515"
USIKILIZE WIMBO WAO HAPO KUSHOTO (ShowBiz Hitz).

Read More......
Sunday, January 23, 2011 Posted in | | 0 Comments »

King katika pozi la kifalme
Ghetto King
King (kulia) na Producer Villy wa 24/7 Records
King (kulia) na Producer Athur wa Aegies Records
King studio

Kutoka pande za Kawe, Dar mchizi aliyeanza mishemishe za game ya muziki wa kizazi kipya kitambo, Saimon a.k.a Sai Dog au Ghetto King ameweka pezani plani zake kwa mwaka huu wa 2011.
Akisema na ebwanadaah, King alifunguka kwamba kwa kuanza tayari amedondosha video ya ngoma yake mpya yenye jina la Birthday ambayo imefuatiwa na audio yenye jina la Wanapagawa aliyowapa shavu Temba na Jos Mtambo wa Kigambonino ambayo imegongwa ndani ya studio za 24/7 chini ya prodyuza Villy.
"Wanapagawa itafuatiwa na video yake itakayoanza kufanyiwa kazi hivi karibuni kupitia Limire Production chini ya muongozaji Malcom. Kingine hivi sasa tunajipanga kuja na family itakayokuwa na vichwa vinne na madensa tisa wa ukweli ambayo tutaitambulisha hivi karibuni kila kitu kitakapokuwa tayari," alisema King ambaye jana alisheherekea siku yake ya kuzaliwa baada ya kutimiza miaka kadhaa duniani.

Read More......
Posted in | | 0 Comments »

Mchizi aliyekuja vizuri katika sanaa ya muziki wa kizazi kipya, Godzilla jana alinusurika kufa baada ya kupigwa mzinga na ndinga alipokuwa kwenye Bajaj na mchizi wake wakielekea kunako studio za 24/7 zilizopo pande za mikocheni kwa Warioba.
"Tulikuwa kwenye Bajaj tukielekea studio ghafla tukashtukia tumepigwa kwa nyuma na gari, ajali ambayo ilisababisha nivunjike jino moja na majeraha mengine mdomoni, ila nashukuru Mungu hatukupoteza uhai. Hivi sasa tupo kituo cha polisi Oysterbay kwa maelezo zaidi," alisema Zilla ambaye kabla ya tukio hilo alikuwa akijiandaa kuutambulisha umoja wao, Zilla Inc.

Read More......
Posted in | | 0 Comments »

Janja stejini
...hapa akiwa juu ya mkoko
..hapa akishangaa

Dogo anayekuja juu kukako game ya muziki wa kizazi kipya kutoka pande za A-Town, Abdul a.k.a Dogo Janja juzikati alijikuta katika wakati mgumu baada ya kuitungua bajaj kwa nyuma na kusababisha mtafaruku kwa saa kadhaa.
Ishu hiyo ilichukua nafasi maeneo ya Sinza, Dar wakati dogo alipokuwa akisukuma mkoko (gari) na kujikuta akiingia nyuma ya bajaj ambapo baada ya mzozo wa hapa na pale na raia waliyokuwa pande hizo askari polisi waliingilia kati na kuihamishia kesi hiyo kituoni.
Akipiga stori na ebwanadaah memba wa kundi la Tip Top Connection, Hamad Ally a.k.a Madee alisema kwamba, baada ya ishu hiyo kutinga mikononi mwa polisi waliingilia kati na kuimaliza kiutu uzima. "Unajua dogo haruhusiwi kuendesha gari barabarani zaidi ya kule kwetu uchochoroni lakini aling'ang'ania aachiwe na mchizi wetu aliyekuwa naye wakielekea Tip Top.
Ndiyo maana tukaiwahi ishu hiyo kabla haijafika mbali. Kosa hilo halitajirudia tena, tutamuweka chini na kumpa darasa kuwa umri wake haumruhusu kuendesha gari".

Read More......
Posted in | | 0 Comments »


"Inakuaje kaka, nimeachia ngoma mpya inakwenda kwa jina la 'Moyo wa Subira', nimegonga na Mona Ganstar ambaye ni prodyuza wa Belle 9. Video yake nafanya Jumapili ya leo na Erly wa ShowBizz, nategemea sapoti kutoka kwako. Linex Sunday Mjeda. 1 blood".

Read More......
Posted in | | 0 Comments »

Ilikuwa ni huzuni kubwa mwishoni mwa wiki iliyopita wakati mfanyakazi mwenzangu Imeld Mtema alipofiwa na mwanaye Precious na mazishi kufanyika katika makaburi yaliyopo maeneo ya Ukonga, Mombasa, Dar. Pichani Imelda (katikati) akisaidiwa kutembea na Mumewe, Dickson pamoja na rafiki yake kipenzi, Tekla (kushoto).
Tukipata chakula cha mchana kabla ya kuaga mwili marehemu
Lilifuata zoezi la kuaga kisha tukaelekea makaburini
Hapa mazishi yakiendelea
Nilipata nafasi ya kuweka shada la maua kwa niaba ya uongozi wa kampuni yetu na wafanyakazi ambao tuko ofisi moja na Imelda.
Mwisho nilipiga picha ya pamoja na wafiwa juu ya kaburi kwa ajili ya kumbukumbu. Bwana alitoa na Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe.

Read More......
Tuesday, January 18, 2011 Posted in | | 0 Comments »


Find more videos like this on TEEN TZ

Read More......
Friday, January 14, 2011 Posted in | | 0 Comments »

Read More......
Posted in | | 0 Comments »

Read More......
Monday, January 10, 2011 Posted in | | 0 Comments »

Read More......
Posted in | | 0 Comments »

Read More......
Sunday, January 9, 2011 Posted in | | 0 Comments »

Thanks Kwa God, Msikilizaji, Mshabiki Na Machizi Wangu Wote Africa Mashariki Kwa Upendo Na Ushirikiano Wenu 2010, Wish You A Happy Successful New Year 2011. In 2011,Sam Misago has been updated to version 6.9.....don,t use the old one!!! To Get The New Version .Power Jams On East Africa Radio 1pm To 4 pm ,Dar es salaam 87.8 ,Mwanza 92.2, Moshi 93.4 ,Arusha 93.6 ,Nairobi 94.7 , Kampala 99.0 , BORN READY.

Kwa mujibu wa Bongo Star Link


Read More......
Monday, January 3, 2011 Posted in | | 0 Comments »