ILI MUZIKI WETU UWEZE KWENDA KIMATAIFA NI LAZIMA TUBADILIKE, SAPOTI YAKO PIA MUHIMU

Berry Black alipokuwa kiwanja
Tangazo la shoo za Berry lilivyokuwa

Kutoka pande za Zenji, msanii Berry Black amesema na ebwanadaah kuwa, taarifa zilizorushwa na kituo kimoja cha redio ya burudani Bongo hivi karibuni kwamba aliburuzwa na promota mmoja aliyemvuta Uingereza kwa malipo kidogo hazina ukweli wowote.
Akipiga stori na blog hii leo kwa njia ya mtandao kutokea visiwani humo staa huyo wa ngoma ya 'Najua' alisema kuwa jamaa walimchana kwamba alipelekwa Uingereza kupiga shoo zaidi ya tano lakini mkwanja aliopewa na promota huyo siyo zaidi ya laki tatu kitu ambacho siyo cha kweli, bali alifanya shoo nne ambazo kila moja alivuta dola za Kimarekani zisizopungua 1500 (Msomaji unaweza kupiga hesabu kwa pesa ya Kibongo)
"Jamaa wanasema kuwa promota alinilainisha kwa maneno kwamba nitaenda kusafisha nyota kwasababu sijawahi kufika pande zile wakati mimi ninachoangalia ni maslahi ya kazi yangu, siyo kuuza sura au kusafisha nyota," alisema Berry.
Hivi sasa mchizi yuko Zenji kwa ajili ya mapumziko baada ya ziara hiyo ndefu, next week anatarajia kushuka kunako jiji la Dar kuendelea na mishe nyingie za kimuziki.

Read More......
Thursday, June 30, 2011 Posted in | | 0 Comments »

Mpango mzima wa pati hii ya video mpya ya Temba na Chegge ulichukua nafasi pande za Mikocheni kwa Felisian Mutta
...Hapa pati ikiendelea huku video ikichukuliwa na Adam Juma wa Visualab (hayupo pichani)
Mkubwa Fella, Chegge, Temba wakibadilishana mawazo wakati zoezi likiendelea

Mimi pia nilishoo love na Shalomilionea (Shalobalo) ambaye alikuwa steringi wa video hiyo
Mkubwa Fella na YP aliyerudi kundini TMK hivi karibuni
Chegge, Ferooz, Temba wakipozi kwa mapumziko ya muda kabla mzigo haujaendelea
Hawa ni Temba na Stiko wa TMK Family
Mimi na Anti Lulu
Ferooz na Anti Lulu pia ulikuwa mpango mzima
Mimi na Chegge
HIZI ZOTE NI POZI ZA ANTI LULU


KAMATA MWIIIIZI MEEEEEEEEN!

Juzi kati vijana wawili kutoka TMK Wanaume Family, Temba na Chegge walikuwa taiti wakigonga video ya ngoma yao mpya, 'Kama ni Gangstar' waliyompa shavu Ferooz. Zoezi lilichukua nafasi pande za Mikocheni kwenye hekalu la Mzee Felisian Mutta na kuwahusisha mastaa na warembo kibao wa Kibongo, huku Adamu Juma wa Visualab akihusika kutengeneza mzigo huo. Kazi inatarajiwa kwenda hewani siku chache zijazo. Kaa mkao wa kula.

Read More......
Saturday, June 18, 2011 Posted in | | 0 Comments »

Kama nilivyokuahidi siku kadhaa zilizopita kwamba, nitavuta waya mpaka pande za Geita, Mkoani Mwanza na kucheki na msanii Godfrey Tumaini 'Dudubaya' ili aweke wazi kuhusiana na skendo yake ya kutupwa selo kama ilivyoripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari hivi karibuni.
Akipiga stori na ebwanadaah leo mchana Dudu amefunguka kwamba, ameshangazwa na baadhi ya vyombo vya habari kuripoti kuwa alitupwa selo na kulala ndani wakati ukweli ni kwamba alipofikishwa kituoni hapo alijidhamini na kuachiwa huru siku hiyo hiyo.
“Da! Nimeshangazwa sana na baadhi ya vyombo vya habari kama magazeti ya…..(anayataja) kwa kuandika kuwa nilikamatwa na kuswekwa lupango wilayani Geita ambamo nililala hadi asubuhi, ishu ambayo siyo kweli. Pia nimegundua kuwa waandishi wengine wa habari huwa hawawatendei haki wahusika kwasababu hakuna aliyenipigia na kuniuliza kilichotokea bali wao waliandika wanavyojua baada ya kusikia uvumi kwa watu ili mradi wanidhalilishe tu.
“Ni kweli nilikuwa nadaiwa shilingi 250,000 (laki mbili na nusu) na promoa mmoja huku Geita, ilikuwa ni kwa ajili ya kufanya shoo kwenye mkesha wa mwaka mpya yaani mwaka jana mwishoni lakini kutokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo wangu nilishindwa kutokea kwenye shoo yake. Hivi karibuni nilipoibuka pande hizi kwa ajili ya shoo jamaa akanitokea na polisi wakanikamata, tulipofika kituoni nikajidhamini kwa shilingi laki moja, siku iliyofuata yaani Mei 31 nikafikishwa mahakamani ambako nilishauriwa nilimlipe jamaa mkwanja wake ili tumalizane kwa amani.
“Nilikubaliana na hilo, tukapanga tumalizane mwezi huu tarehe 23 ambapo nitampa lakini moja na nusu iliyobaki. Ukweli ni kwamba hata kama ningekuwa sina pesa mfukoni nisingelala selo kwasababu huku Geita kuna kaka zangu wanafanya kazi mgodini, waliposikia niko polisi walikuja na balozi wa mtaa wao kwa ajili ya kunichukulia dhamana. Nimeshangazwa sana na stori za mimi kulala selo, nafikiria kitu cha kufanya ili tabia kama hii ya kudhalilishana kwenye vyombo vya habari bila sababu isijirudie tena kwa watu wengine”, alifunguka Dudu a.k.a Mamba.

Read More......
Friday, June 10, 2011 Posted in | | 0 Comments »

Hii ni ngoma yangu mpya baada ya ile ya Hadithi, yaitwa 'Narudi Nyumbani', nimewashirikisha Cheleaman na Zuhura, kazi imefanyika Bamba Rec iliyopo Mbezi, Kibamba chini ya Producer Mobbaizoh aliyegonga ngoma ya Dongo Janja yenye jina la 'Anajua'. kazi hii tayari ipo katika baadhi ya vituo vya redio huku nikifanya maandalizi ya video yake. Nafahamu. Huu ni muendelezo wa kazi zangu za muziki mpaka kukamilisha albamu yenye jina la Historia ambayo itakuwa na nyimbo 8, bado kazi 3 ikamilike. Asante kwa sapoti yako mdau. Waweza kuisikiliza ngoma hapo juu kushoto.

Read More......
Monday, June 6, 2011 Posted in | | 0 Comments »

K-Sher katika pozi
Msanii Khadija Shaban ‘K-Sher’ a.k.a Mama Jamkay ametambulisha ngoma mpya yenye jina la 'Hamu' ukimshirikisha Marlaw akimaanisha kwamba baada ya kimya kirefu a.k.a likizo ya uzazi sasa anarudi tena sanaani ili kuendeleza pale alipoishia wakati anafanya vizuri na nyimbo kama Uvumilivu na Tunda. Binafsi huwa nazikubali kazi zake ni nimeipokea kwa mikono miwili traki hii itakayofuatiwa na video yake, wewe je?

Read More......
Posted in | | 0 Comments »



Ishu iliyodondoka ndani ya Ebwanadaah hivi karibuni inahara kwamba, staa wa Bongo Muvi na muziki wa kizazi kipya, Hemed Suleiman na mshindi wa pili wa shindano la Tusker Project Fame mwaka jana, Peter Msechu wameitwa kwa ajili ya kujiunga na washiriki wengine katika muendelezo wa shoo hiyo itakayofanyika pande za Nairbi nchini Kenya.
Unajua nini kilichowafanya washikaji wapate zali kwa mara ya pili? Kwasababu mchongo mzima utakwenda kwa jina la Tusker Project Fame All Stars na unawahusu wale washiriki waliyowahi kufanya vizuri kwenye mashindano yaliyopita kama ilivyokuwa kwenye mpambano wa Big Brother mwaka jana.
Kitakachofuata baada ya washiriki wa Tusker kuanza kwenda hewani ni kura zitakazowawezesha kuibuka na ushindi. Jiandae.

Read More......
Posted in | | 0 Comments »



Katika kuonesha kwamba bado anaisimamia vyema sanaa yake, Dudubaya a.k.a Godfrey Tumaini amerudi na kioo kipya (video) huku akiwa bado amepiga kambi Kanda ya Ziwa akisikilizia michongo. Kuhusiana na ishu yake ya kutupwa selo huko pande za Geita, Mwanza ntamtafuta ili aweke kila kitu wazi kupitia hapa ebwanadaah.

Read More......
Posted in | | 0 Comments »

Kutoka pande za Mwanza Mwanza, msanii na mtangazaji wa redio, Phiribert Kabago ameanza kuonekana luningani ni video ya ngoma yake, Umeme wa Mgao iliyosimamiwa korasi na mwanadada Farida.
Kazi imefanyika chini ya Kinye Media ya Mwanza chini ya mtayarishaji Kinye. Lokesheni kama Igoma ilipo mitambo ya Tanesko imetumika zaidi kwenye kioo hicho li kuleta uhalisia, yakiwemo matukio yanaoowaonesha baadhi ya Wabongo waliyopata matatizo kutokana na kukithiri kwa mgao wa umeme. Big Up kijana kwa kuipigania jamii iliyokuzunuka.

Read More......
Posted in | | 0 Comments »