ILI MUZIKI WETU UWEZE KWENDA KIMATAIFA NI LAZIMA TUBADILIKE, SAPOTI YAKO PIA MUHIMU

Mimi (kushoto) na prodyuza Deez wa Bamba records tukiwakilisha na tshirt za BADUGU

Mimi na Zuhura (Shosti)

Dansa MC V akijiandaa kurekodi kipande chake
Zuhura, Mimi, prodyuza, Mobbyzow, Deez na densa aliyekuja kutupa sapoti
Mdau wangu wa karibu, Zuhura na Mobbyzow
Director, Chief (kushoto) Zuhura na msanii Faby J
Hili ni pozi la dansa wangu, MC V baada ya kumaliza kushoot

Niaje wadau, mkoa poa? Kwanza kabisa nachukua nafasi hii kuwaomba radhi kwa kuwa kimya kwa muda, ila waswahili husema, Kimya kingi kina mshindo mkuu, nilikuwa tait kunako mishemishe za kumalizia video ya ngoma yangu 'NARUDI NYUMBANI' niliyowashirikisha Zuhura na Cheleaman ambaye kwasababu zilizokuwa nje ya uwezo wake hakuweza kuonekana kwenye video hii (kama mnavyoona pichani). Nashukuru Mungu mzigo umekamilika na tayari umeshaanza kwenda hewani kupitia vituo kadhaa vya televisheni. Thanx kwa director wangu, Tonee na jembe lake, Chief bila kuwasahau prodyuza wangu, Mobbyzow wa Bamba Records, Deez, shost wangu Zuhura, dansa wangu MC V na wote walioshiriki kufanikisha mpango huo. Mungu awabariki sana, naombeni sasa tuwaachie kazi Watanzania ambao ndiyo majaji, naamini watatupokea vizuri pamoja na familia tuliyoianzisha, 'BADUGU NATIONAL'
ASANTENI KWA SAPOTI YENU.

Read More......
Wednesday, November 23, 2011 Posted in | | 0 Comments »

Bi. Kidude
Mkongwe za muziki wa taarabu pande za Zenji, Kidude Binti Mbaraka a.k.a Bi. Kidude leo amekanusha vikali uvumi ulionea kwamba amefariki dunia.
Akikanusha kwa mbwembwe zote, Bi. Kidude alisema kwamba yeye bado yuko hai na nguvu za kutosha, isipokuwa alikuwa akisumbuliwa na homa ya kawaida na kulazimika kutundikiwa dripu ya maji, lakini sasa afya yake imetengemaa.
Kutoka Ebwanadaah: Jamani Wabongo wenzangu, haya mambo ya kusambaza taarifa ambazo hatuna uhakika nazo siyo fresh, ipo siku itatukosti. Zaidi tuendelee kumuombea bibi yetu azidi kuwa na afya njema.

Read More......
Wednesday, October 26, 2011 Posted in | | 1 Comments »


Mambo vipi?

Jackson Makini aka CMB PREZZO kutoka nchini Kenya amedondosha kazi mpya 4 SHO 4 SHIZZY aliyomshirikisha Producer wa ngoma hiyo ULOPA kutoka katika studio ya SAMAWATI ya Jijini Nairobi Kenya,Video ya kazi hii ameshoot na kampuni ya BOOMBA Video inatarajiwa kutoka baada ya wiki mbili katika vituo vyote vya Tv Africa nzima:

Pamoja sana

Ambwene Yessayah (AY)


Read More......
Tuesday, October 25, 2011 Posted in | | 0 Comments »

Enzi za uhai wake
Baada ya kuuawa

Taarifa zilizoifikia Ebwanadaah hivi punde kutoka kunako televsheni za kimataifa zinasema kwamba aliyekuwa Rais wa Libya, Muhamar Gadaffi ameuawa na majeshi ya waasi kama inavyoonekana pichani. Mengi zaidi kuhusu kifo chake endelea kucheki na blog hii.

Read More......
Thursday, October 20, 2011 Posted in | | 0 Comments »

Hii ni moja kati ya shoo zao huko Botwana
Mmoja wa waimbaji na dansa wa kundi hilo
Dikakapa waliposhuka Airport Juzi alfajiri

Kundi lingine maarufu la muziki wa asili kutoka Botswana, Dikakapa limedondoka Bongo juzi alfajiri kwa ajili ya shoo za kutosha, huku likitamba kuwa litafanya maajabu na ikiwezekana kuwapoteza Makhirikhiri waliowahi kuja TZ na kupiga shoo zaidi ya miezi kadhaa.

Read More......
Wednesday, October 12, 2011 Posted in | | 0 Comments »


Mtoto Sesilia (katikati) akiwa na mtangazaji wa Kipindi cha Mimi na Tanzania, Hoyce Temu (kulia) na mlezi wake, Nyarugembe Peter Kambaliko (kushoto)


Ndugu Watanzania,

Jumapili tarehe 11 Septemba, kipindi cha Mimi na Tanzania kinachorushwa hewani na kituo cha luninga cha Chanel Ten, kilifanya mahojiano na mtoto Sesilia Edward (14) anayesumbuliwa na matatizo ya moyo, ambaye anahitaji kufanyiwa upasuaji wa haraka ili kuokoa maisha yake. Upasuaji huo unatakiwa kufanyika nchini India,

jumla ya dola 15 (sawa na shilingi milioni 24) za kitanzania zinahitajika kuokoa maisha yake. Kama asipofanyiwa upasuaji huo wa haraka atapoteza maisha ndani ya mwezi mmoja.

Baadhi ya Watanzania wameanza kuchangia ili kumsaidia mtoto Sesilia kupitia katika simu za msamaria mwema anaeishi naye huko Mbagala, Bw. Nyarugembe Peter Kambaliko katika nambari zifuatazo:



Tigo Pesa:- 0715 095797

MPESA: – 0762 962467

NMB Account: 2072517079


Hadi sasa zaidi ya shilingi milioni mbili zimeshachangwa, bado michango inaendelea kupokelewa.

Watanzania wenzangu, kutoa ni moyo, usambe si utajiri.


Mtoto huyu ni Mzaliwa wa Kisarawe, yatima na anishi na mlezi aliyemkuta akiwa taabani nyumbani alikokua akiishi na dada anayejishughulisha na shughuli za vibarua vya kulima mashamba ya watu. Alitakiwa kufanya mitihani ya Darasa la Saba na wenzake mwaka huu lakini hali yake haikumruhusu. Ndoto zake ni kuwa mwalimu.


Mlezi wake Peter Nyarugembe, amejaribu kuzunguka katika hospitali mbalimbali bila mafanikio.


Asanteni sana kwa kuokoa maisha ya Sesilia.

Read More......
Thursday, September 15, 2011 Posted in | | 0 Comments »

PETER MSECHU (TANZANIA) - WINNER TUSKER ALL STARS - 2011

Shindano la Tusker All Stars lililoanza 26 June,2011 limefikia fainali jana tarehe 14 August,2011 kwa washindi watatu kupatikana

Alpha Rwirangira toka Rwanda (TPF 3 - Winner),Peter Msechu toka Tanzania (Mshindi wa 2 – TPF 4) na Davis Ntare toka Uganda (TPF 4 – Winner) wameibuka washindi na wamepata shavu la kupiga show same stage na wasanii wa kimataifa baadaye mwaka huu nchini Kenya....

Washiriki wengine walikua Hemedi Suleiman toka Tanzania,Caroline Nabulime na Amileena Mwenesi toka Kenya,Bernard Ng'ang'a na Patricia Kihoro toka Kenya walishiriki na walikaa wiki 8 na Ma Mc walikua ni Prezentaz maarufu Eve D'Souza toka Kenya na Gaetano Kagwa toka Uganda na mbali na washindi hao 3 kupata shavu la ku-share stage moja na wasanii wa kimataifa,haijafunguliwa kama watapata zawadi au vp....!

Kwa hisani ya Bongostarlink.

Read More......
Monday, August 15, 2011 Posted in | | 0 Comments »

Madee
Ney

Mastaa wa game ya Bongo Flava, Madee a.k.a Hamad Ally na Ney wa Mitego a.k.a Emmanuel Elibarick wameshiriki katika ngoma moja yenye jina la Twende Sawa inayozungumzia baadhi ya matatizo yanayolikabili Taifa letu ukiwemo mgao wa umeme unaoendelea hivi sasa na kuwafanya Watanzania wengi wanaotumia nishati hiyo kujingizia kipato kushindwa kufikia malengo yao huku wengine wakizidi kuyumba kiuchumi na familia zao.

Hiyo ni ngoma yangu mpya 'GEORGE MC' ambayo nimewashirikisha mastaa hao ambao katika hali ya kawaida hawawezi kufanya kazi pamoja kutokana na tofauti zao kimuziki, lakini walikubali kushea nami idea kwasababu ya uchungu walionao kwa Wabongo wenzao wanaoendelea kupiga maktaim wakishindwa kuyafikia maisha bora kutokana na janga la umeme.

Kazi hiyo ambayo imefanyika Bamba Rec, chini ya mtayarishaji, Mubbyzoh tayari imeshadondoka kitaani pamoja na kwenye baadhi ya vituo vya redio ndani na nje ya Dar es Salaam (Pia unaweza kuisikiliza hapo juu kushoto kwenye ShoBiz). Ndugu zangu wasanii, huu siyo wakati wa kufurahishana wakati Watanzania wengi hivi sasa wanapita katika kipindi kigumu cha maisha kwa matatizo kibao yanayoendelea kuikumba nchi yetu, sisi kama kioo cha jamii tunasimama vipi na jamii wakati huu?. Thanx Madee na Ney wa Mitego kwa kukubali kusimama pamoja nami katika kuwafikishia ujumbe wananchi na wahusika wa matatizo hayo.

Kumbukeni kwamba vijana ni taifa la leo siyo la kesho na msiba wa leo huwezi kuwa na uchungu na kulia keshokutwa wakati matanga yameshaanuliwa.


Read More......
Posted in | | 0 Comments »


Kutoka ndani ya kundi la Wachuja Nafaka lililofufuka upya hivi karibuni, msanii Juma Kassim Kiroboto 'Nature' amesema kwamba kamwe hawezi kupiga mzigo na studio ya Shalobalo inayomilikiwa na kijana Bob Junior.
Nature alitamka hilo jana usiku kupitia kipindi cha Friday Nighty Live (FNL) kinachorushwa hewani kila siku ya Ijumaa kupitia kituo cha televisheni ya Channel 5 baada ya kugongwa swali na mtangazaji Samuel Misago kwamba kuna siku atakwenda kufanya kazi Shalobalo Rec?
"Haitatokea hata siku moja kufanya kazi na hao madogo, siwezi kufanya muziki tofauti na ninavyotaka mimi, wao hivi sasa wako juu lakini na sisi kama wakongwe tuko juu ile mbaya. Tumeitoa mbali sana hii game, tulikuwa tunatembea umbali mrefu kwa ajili ya kwenda kurekodi" alisema Nature huku akisisitiza kamwe mtu hawezi kumlazimisha akarekodi Shalobalo.

Read More......
Saturday, July 16, 2011 Posted in | | 0 Comments »


Msanii Langa Kileo amefunguka kwamba baada ya kuzama katika utumiaji wa dawa za kulevya na kuamua kuachana nazo hivi karibuni anataka jamii imtambue kama Rais wa Mateja ambaye atakuwa mfano mzuri kwa wenzake ambao bado wanaendelea kutumia.
Langa alisema kuwa miaka kadhaa iliyopita alijikuta akizama katika utumiaji wa dawa hizo baada ya kugongea fegi iliyokuwa imemiksiwa na drugs kutoka kwa mshikaji wake na alipovuta tayari stimu zikawa zimemuingia na kumfanya aendelee kubembea hadi hivi karibuni alipoamua kujivua gamba la uteja.
"Ilifikia wakati nikahama nyumbani japo kimaisha mzee yuko poa na kwenda kuishi kwenye mageto ya washikaji tukipiga dili za kuvuta unga na kuiba. Nilikonda na kupoteza nguvu kabisa, ilibaki hatua ya mwisho kwenda kupiga debe kwenye vituo vya daladala, lakini nashukuru Mungu nimefanikiwa kuchomoka huko.
"Wengi ambao bado wanaendelea kutumia watajiuliza nimewezaje kuachana, wapo watakaonionea wivu kwa hilo kwasababau ni kazi ngumu kidogo kujiondoa katika kundi hilo, ila nitaendelea kufanya kampeni za kuwahamasisha wengine pia kuacha kwani inawezekana," alisema.
Ebwanadaah inampongeza Langa kwa ujasiri huo na kumuombea kwa Mungu afya yake izidi kuwa poa kwani jamii bado inahitaji kupata elimu kupitia ngoma zake.

Read More......
Posted in | | 0 Comments »



Niaje wadau wa ebwanadaah? Kutokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo nilishindwa kuipost taarifa hii ya Sugu kwa muda na tarehe iliyotoka, lakini siyo mbaya kwa wale ambao hawajaipata wakaisoma leo kupitia hapa.


"Jana tarehe 8 Julai 2011 Polisi walinikamata kwa kile walichokiita kuwa ni kufanya mkutano bila kibali.
Hata hivyo, mtiririko wa matukio unaonyesha kwamba polisi walisukumwa na sababu nyingine kwa kuwa suala la taarifa kupelekwa polisi kama sheria zinavyohitaji lilishashughulikiwa na viongozi wa CHADEMA mkoa na wilaya ya Mbeya Mjini.
Leo tarehe 9 Julai 2011 pamoja na kutolewa kwa dhamana polisi wameonyesha nia ya kutaka kuzuia tamasha la wazi la bure ( ‘Burudani Nyumbani’) ambalo wasanii mbalimbali walikuwa walifanye kwa mwito wangu kwa ajili ya kutoa burudani na kuhamasisha maendeleo. Polisi wameonyesha vitendo vya kutaka leo kufanyike tamasha la fiesta pekee wakati ambapo matamasha haya yote mawili yameandaliwa na wadau tofauti katika maeneo tofauti.
Mpaka wakati huu ninapotoa taarifa hii wananchi wengi wamejikusanya katika uwanja wa Ruanda Nzovwe ambao ni maarufu kama Uwanja wa Dr Slaa wakisubiri tamasha hilo lakini polisi wameonyesha dhamira ya kutaka kuwatawanya.
Maneno na vitendo vya Jeshi la Polisi vinaelekea kuwa na uhusiano na kauli ambayo niliitoa hivi karibuni kupitia mtandao wa Facebook ya kutohitaji tamasha la Fiesta kufanyika Mbeya.
Katika mazingira haya ni muhimu nikaeleza tu kuwa kauli yangu kuhusu Fiesta ilikuwa na madhumuni ya kuanzisha mjadala kuhusiana na suala zima la wizi na unyonyaji uliopo kwenye Sanaa, ambao sio tu unawanyima haki Wasanii, bali pia kukosesha mapato kwa Serikali ambayo yangetokana na kodi kupitia Sanaa ikiwemo muziki.
Nilifanya hivyo baada ya tamasha hilo kutangazwa kufanyika katika eneo ambalo wananchi wamenipa wajibu wa uongozi wa kuwatumikia na kuwawakilisha. Hivyo kwa niaba ya wananchi wa Mbeya Mjini wanaokosa mapato katika sanaa na wasanii wa Mbeya wanaokosa fursa kutokana na vikwazo nilichukua uamuzi wa kuwakilisha kupaza sauti kama ambavyo nimekuwa nikipaza sauti katika masuala mengine yanayogusa umma kama viwanda, kilimo, barabara za Mbeya Mjini na Haki za wanafunzi wa Elimu ya Juu pamoja na makundi mengine katika jamii.
Niliamua kupaza sauti katika hili kupitia Fiesta, kwa kuwa waandaji wake kimsingi ni sehemu ya vyanzo vya maovu kwenye maendeleo ya muziki hapa nchini. Fiesta ikiwa kitovu cha uonezi kwani hata Wasanii wanaoshiriki halipwi ipasavyo au hawalipwi kabisa. Na hii ni kutokana na wao kutumia njia haramu kuhodhi (monopolise) biashara ya muziki hapa nchini, huku wakiwanyima nafasi watanzania wengi kutumia vipaji na ubunifu wao kwenye biashara ya muziki.
Waandaji wa Fiesta ndio wenye redio ya Clouds, Kampuni ya promotion ya Primetime, na pia wanahusika na N.G.O ya THT, waandaji wa matamasha ya injili, ikiwemo kuwa na ushirika katika Tamasha la Pasaka.
Huku wakiwa na ushawishi wa hila kwenye Kili Music Awards (One Call Promotion) na mambo mengine yote muhimu yanayohusu Sanaa. Ikiwemo ujumbe wa bodi kwenye Tamasha la majahazi, Zanzibar. Lisingekuwa jambo baya kama wangetumia nafasi hizo kwa haki na maendeleo ya sanaa. Kutokana na haya, kwa miaka mingi himaya ("empire") hii imetumia nafasi yake dhalimu kukandamiza watu wengine hasa Wasanii. Kwa mfano kama Msanii hayupo kwenye hiyo "himaya" yao basi hana nafasi ya kutimiza ndoto yake. Na iwapo Msanii hakubaliani na taratibu zao au malipo finyu wanayowalipa Wasanii, basi watahakikisha wanampiga vita na hatimaye kuhujumu usanii wake ili atoweke, kwa kuwa tu hakubaliani nao. Msanii hana haki ya kufanya majadiliano ya kibiashara mbele yao.
"Empire" hii imehodhi mpaka makampuni ya udhamini hapa nchini, ambapo makampuni haya yamekuwa magumu kutoa udhamini kwa wadau wengine kwa kuwa tu wao ni washirika wa "Empire" hii.
Walifikia hatua ya kuhodhi mpaka biashara ya usambazaji kwa "Wadosi" ambapo bila ya wao kuruhusu basi Msanii yeyote kazi yake haipewi nafasi ya kusambazwa wala kusikika. Hata kama nyimbo au album yake ni nzuri kwa kiasi gani.
Kibaya zaidi wamehodhi mpaka nia njema ya Rais Kikwete katika kusaidia Sanaa na Wasanii. Mfano ni Studio ambayo Rais kupitia Bunge Tukufu la Jamhuri ya Muungano alitangaza kuwa amewapa Wasanii wa Tanzania, lakini baadaye tukashangaa kusikia ipo mkononi! Pia Rais aliahidi na kutoa nyumba ya Serikali kwa Wasanii ambayo ingetumika kuendeshea Studio husika, lakini nyumba hiyo ya Serikali iliyotolewa na Rais sasa iko chini yao na ndio makao ya THT! Wamefanikiwa kumhadaa Rais kuwa wao ndio "Care takers" wa Sanaa ya Tanzania akawaamini na wao wanaitumia vibaya imani njema ya Rais kwao kufanya dhuluma. Yote niliyoyataja juu, japokuwa hayo ni kwa uchache tu! Yanalalamikiwa sana na wasanii wengi na wadau hapa nchini, japokuwa wengi wameshindwa kujitokeza waziwazi kutoka na vitisho vya watu hawa.
Vitendo hivyo wanavyofanya vimeleta madhara katika tasnia ya sanaa na matokeo yake ni kudumaa kwa maendeleo ya muziki hapa nchini. Vijana wengi wanaojihusisha na sanaa wamepoteza matumaini. Wengi walipata tegemeo la ajira kupitia muziki, lakini hali haipo hivyo tena. Vijana wengi wasanii wamekata tamaa kwa ajili ya ukandamizaji wa "empire" hii.
Na sio tu wasanii na wadau wengine wanawapoteza katika hili. Kwa watu hawa kuhodhi na kuvuruga kabisa biashara ya muziki, hata Serikali inapoteza fedha nyingi kupitia kodi. Kwa mujibu wa utafiti wa Dr. Jehovaness Aikaeli ambaye ni mchumi wa UDSM, hata katika hali hii mbaya ya biashara ya muziki, Serikali imepoteza Tsh. Milioni 18, kwa kutokusanya kodi kupitia muziki tu, ukiachilia mbali filamu na sanaa nyingine. Na iwapo hali itaboreshwa basi kodi hiyo itapanda mpaka wastani wa Tshs. Bilioni 50 kwa mwaka! Hizi sio pesa kidogo kwaserikali, hasa ukizingatia bajeti ya Wizara inayohusika na Utamadnuni ni Tsh bilioni 14, kwa mwaka, fedha ambazo mara nyingi hawapewi zote kutokana na Serikali kutokuwa na fedha ya kutosha! Lakini hapa utaona kukwa kodi ya mwaka peke yake ingetosha kwa bajeti ya Wizara na ziada kubwa ingebaki kwa miradi ya maendeleo kama kujenga Art Theatres n.k
Napenda ieleweke wazi kwamba mimi binafsi ni "Mhanga" au "victim" wa uharamia wa "himaya" hii kwa miaka mingi, tukupitia migogoro kadhaa ya kibiashara lakini kilichonisikuma kuchukua hatua hii; sio nafsi yangu pekee bali wajibu nilionao hivi sasa kama mwakilishi umma.
Izingatiwe kuwa baada ya mimi kuchaguliwa kuwa Mbunge na wananchi wa Mbeya tena kwa kishindo, Serikali kupitia Wizara inayohusika na utamaduni na pia Baraza la Sanaa (BASATA), walinipongeza kwa barua huku wakinitaka niendelee na harakati za kupigania sanaa na wasanii kwa kutumia nafsi au jukwaa langu jipya Bungeni na nje ya Bunge. Jukumu ambalo nililikubali kwa mikono miwili kwani harakati za muziki huu si kitu kipya kwangu, ulianza kabla ya Ubunge na ndio ninachokifanya na hasa ukizingatia mimi pia sasa ni Waziri Kivuli (Shadow Minister) wa Wizara ya Habari, Vijana na Michezo.
Kwa lugha nyingine ujumbe nilioutoa wa kukataa Fiesta ni ishara ya mgomo wenye nia ya kutuma ujumbe wa madai ya msingi. Na historia inaonyesha kuwa, Wasanii wa Nigeria walianza kulipwa vizuri kama wanavyolipwa sasa baada ya kuanzisha migomo dhidi ya mapromota wanyonyaji wa nchini kwao.
Na kama ni suala la kukuza uchumi na ajira, Ni nini mchango wa Fiesta na matamasha mengine kwa halmashauri za mji na majiji wanayopita na kuvuna mamilioni ya fedha kila siku?
Wenu katika kutaka haki".


Joseph Mbilinyi (Mb)
9/7/2011-Mbeya Mjini

Read More......
Wednesday, July 13, 2011 Posted in | | 0 Comments »

Inspector Haroun
Gangwe ya miaka hiyo ilipokuwa mzigoni
Hii ilikuwa albamu ya mwisho wa Gangwe Mobb kabla ya kusambaratika na kurudi tena mwaka huu

Baada ya kutengana kwa muda mrefu hatimaye wasanii Haruna Kahena 'Inspector Haroun' na Kalama Bakari Jongo "Luteni Kalama' wameamua kuurudisha umoja wao, Gangwe Mobb huku wakitambulisha kwa ngoma yenye jina la Wabishi wa mtaa waliyompa shavu kijana, Godzilla.
"Gangwe imerudi kwa nguvu zote ikiwa kama kampuni iliyosajiriwa, ambayo mbali na muziki itakuwa na miradi mingine kibao ili kuipa nguvu zaidi", alisema Kalama mbele ya Ebwanadaah.

Read More......
Tuesday, July 5, 2011 Posted in | | 0 Comments »

A.Y na mtoto wa Master P, Lil Romeo

Hapa akijiachia na wenyeji wake
Staa wa muvi Hollywood, Megan Good pia alihusika kwenye video hiyo

"HALI VIPI?

"Hii ilikuwa siku tuliyokuwa tunashoot video mpya inayokwenda kwa jina la SPEAK WITH YOUR BODY - AY FEAT ROMEO & LA'MYIA

LOCATION:HOLLYWOOD CALIFORNIA
DIRECTOR: WILLIAM TIKKI & SHAI KEDEM
AUDIO PRODUCED BY: RILEY
GUESTS: NO LIMIT SOLDIERS, ACTRESS MEAGAN GOOD & ACTOR SAM JONES III
VIDEO INATARAJIA KUTOKA BAADA YA WIKI MBILI"

Kutoka Ebwanadaah; Big up mtu mzima Ambwene, tunasubiri mapinduzi kwenye muziki wetu, wengine pia tufuate.

Read More......
Posted in | | 0 Comments »

Hii ndiyo sehemu ya kuingilia ndani ya Banda la Princeware Africa LTD

Baadhi ya wateja wakichagua bidhaa ndani ya Banda la Princeware Africa katika Maonyesho ya Sabasaba yanaoyendelea ndani ya Viwanja vya MWL JK Nyerere, Kilwa Road DSM






Mmoja wa wafanyakazi wa Duka la Princeware akiwa kazini sabasaba




Bidhaa za Princeware zinavyoonekana kwa mbele














Read More......
Saturday, July 2, 2011 Posted in | | 0 Comments »

Berry Black alipokuwa kiwanja
Tangazo la shoo za Berry lilivyokuwa

Kutoka pande za Zenji, msanii Berry Black amesema na ebwanadaah kuwa, taarifa zilizorushwa na kituo kimoja cha redio ya burudani Bongo hivi karibuni kwamba aliburuzwa na promota mmoja aliyemvuta Uingereza kwa malipo kidogo hazina ukweli wowote.
Akipiga stori na blog hii leo kwa njia ya mtandao kutokea visiwani humo staa huyo wa ngoma ya 'Najua' alisema kuwa jamaa walimchana kwamba alipelekwa Uingereza kupiga shoo zaidi ya tano lakini mkwanja aliopewa na promota huyo siyo zaidi ya laki tatu kitu ambacho siyo cha kweli, bali alifanya shoo nne ambazo kila moja alivuta dola za Kimarekani zisizopungua 1500 (Msomaji unaweza kupiga hesabu kwa pesa ya Kibongo)
"Jamaa wanasema kuwa promota alinilainisha kwa maneno kwamba nitaenda kusafisha nyota kwasababu sijawahi kufika pande zile wakati mimi ninachoangalia ni maslahi ya kazi yangu, siyo kuuza sura au kusafisha nyota," alisema Berry.
Hivi sasa mchizi yuko Zenji kwa ajili ya mapumziko baada ya ziara hiyo ndefu, next week anatarajia kushuka kunako jiji la Dar kuendelea na mishe nyingie za kimuziki.

Read More......
Thursday, June 30, 2011 Posted in | | 0 Comments »

Mpango mzima wa pati hii ya video mpya ya Temba na Chegge ulichukua nafasi pande za Mikocheni kwa Felisian Mutta
...Hapa pati ikiendelea huku video ikichukuliwa na Adam Juma wa Visualab (hayupo pichani)
Mkubwa Fella, Chegge, Temba wakibadilishana mawazo wakati zoezi likiendelea

Mimi pia nilishoo love na Shalomilionea (Shalobalo) ambaye alikuwa steringi wa video hiyo
Mkubwa Fella na YP aliyerudi kundini TMK hivi karibuni
Chegge, Ferooz, Temba wakipozi kwa mapumziko ya muda kabla mzigo haujaendelea
Hawa ni Temba na Stiko wa TMK Family
Mimi na Anti Lulu
Ferooz na Anti Lulu pia ulikuwa mpango mzima
Mimi na Chegge
HIZI ZOTE NI POZI ZA ANTI LULU


KAMATA MWIIIIZI MEEEEEEEEN!

Juzi kati vijana wawili kutoka TMK Wanaume Family, Temba na Chegge walikuwa taiti wakigonga video ya ngoma yao mpya, 'Kama ni Gangstar' waliyompa shavu Ferooz. Zoezi lilichukua nafasi pande za Mikocheni kwenye hekalu la Mzee Felisian Mutta na kuwahusisha mastaa na warembo kibao wa Kibongo, huku Adamu Juma wa Visualab akihusika kutengeneza mzigo huo. Kazi inatarajiwa kwenda hewani siku chache zijazo. Kaa mkao wa kula.

Read More......
Saturday, June 18, 2011 Posted in | | 0 Comments »