ILI MUZIKI WETU UWEZE KWENDA KIMATAIFA NI LAZIMA TUBADILIKE, SAPOTI YAKO PIA MUHIMU

Meneja wa Tip Top, Babu Tale
K-Sher (katikati) akiwa na baadhi ya wakali wa Tip Top
First Lady wa Kundi la Tip Top Connection lenye maskani yake pande za Manzese, Dar es Salaam, Khadija Shaban a.k.a K-Sher amesimamishwa kupiga mzigo ndani ya kundi hilo kwa kipindi kisichojulikana.
Akidondosha stori ndani ya ebwanadaah wikiendi iliyopita Meneja wa kundi hilo, Khamis Tale Tale a.k.a Babu Tale alisema kwamba wamefikia uamuzi huo baada ya K-Sher kuonesha utovu wa nidhamu kitu ambacho kimekuwa kikiwapa usumbufu kwa muda mrefu.
“Mara nyingi K-Sher amekuwa akifanya vitu ambavyo vinaleta usumbufu kwa wenzie, mfano hivi karibuni tulikuwa na shoo Mwanza, yeye alishindwa kufika kwa sababu tulishindwa kupata tiketi ya ndege kwa muda huo, wenzie walikuja kwa basi na kufanya shoo kisha kurudi Dar.
“Tulipofika Dar akawa anadai alipwe pesa za shoo hiyo, huku akitishia kujitoa kundini kama hatukufanya hivyo, siyo hilo tu yapo mengi ambayo msanii huyo amekuwa akiyafanya na kusababisha usumbufu kwa wenzie kitu ambacho kimetusukuma sisi viongozi kuchukua uamuzi wa kumsimamisha mpaka hapo baadaye,” alisema Tale.
Safu hii ilijaribu kumtafuta K-Sher kupitia simu yake ya mkononi ili naye aweke wazi kuhusu hilo lakini mpaka tunakwenda mitamboni hakuweza kupatikana. Tunaahidi tutaendelea kucheki naye, atakapopatikana kila kitu kitakuwa wazi kupitia gazeti la Ijumaa litokalo kila siku ya Ijumaa na hapa ebwanadaah.

Read More......
Sunday, August 29, 2010 Posted in | | 0 Comments »


Hapa akiwa na Omarion

Ebwana Dah wiki hii inarudi tena kwa mwanamuziki wa mbele, Kat DeLuna ambapo kwa mara ya kwanza inafahamika kwamba anaanguka kitandani na Omarion Grandberry.
Staa huyo mwenye umri wa miaka 22, aliyezaliwa Novemba 17, pamoja na umri alionao grafu ya wanaume wake ndiyo kwanza imenaswa mtandaoni kwa mara ya kwanza.
Awali, safu hii iliwahi kuripoti kwamba, mwanamuziki huyo hajawahi kupata kashfa ya kulala na mwanaume kitanda kimoja, lakini sasa safari ndiyo imeenza! Dah!

Read More......
Posted in | | 0 Comments »

Read More......
Posted in | | 0 Comments »

Read More......
Friday, August 27, 2010 Posted in | | 0 Comments »

Read More......
Posted in | | 0 Comments »

Mkali wa ngoma za majonzi kutoka kruu ya Tip Top Connection, Khalid Ramadhani ‘Tundaman’ amesema na ShowBiz kwamba amepokea kwa mikono miwili pongezi anazopewa na baadhi ya mashabiki wake kuhusiana na ubora wa kazi zilizomo kwenye albamu yake mpya iitwayo ‘Hali yangu mbaya, inayosumbua sokoni kitaani hivi sasa, Hemed Kisanda anashuka nayo.
Akiangusha stori na safu hii juzi kati Tunda alisema kwamba amekuwa akipokea simu nyingi kutoka kwa mashabiki zinazompa ‘hala’ kwa utunzi bora wa nyimbo zake.
“Albamu ya Hali yangu mbaya ni elimu tosha kwa jamii kwa jinsi nyimbo zake zilivyokuwa na mafundisho ya kutosha, ndiyo maana napata pongezi. Pia katika albamu hiyo yenye nyimbo kumi kuna ngoma moja inakwenda kwa jina la ‘Uzuri wake’ ambayo nimemuimbia staa wa muvi Bongo, Rose Ndauka,” alisema.
Pia msanii huyo aliweka kweupe kwamba kwa wale wenye maswali kuhusu ndoa yake anatarajia kufanya hivyo mapema Februari mwaka ujao.

Read More......
Posted in | | 0 Comments »

Hapa nikipiga naye stori
...akipozi kitandani

...akibeba mashine yake ya kazi
...hapa akiwa mzigoni, akipulizia rangi nyumba
Pozi lake
Kunzia leo ntakuwa nikiwaletea stori za maisha ya mastaa mbalimbali wa Bongo waliotembelewa na safu ya Mpaka Home Next Level inayopatikana ndani ya Gazeti la Risasi litokalo kila siku ya Jumatano. Kwa kuanza leo huyu hapa staa wa muziki wa Bongo Flava, fundi rangi na mjasiriamali Zuhura Mrisho Watuta.
Sinza Kumekucha, Dar es Salaam ndiyo anapofanya maishi yake, mengi kuhusu yeye cheki na intavyuu hapo chini.
Mpaka Home: Ndani ya mjengo huu ndiyo home au umepanga?
Zuhura: Hapa nimepanga, nyumbani kwetu labisa ni Mwanza maeneo ya Igoma.
Mpaka Home: Unamudu vipi gharama za kodi?
Zuhura: Kazi zangu kama kupulizia rangi, muziki na biashara za vitu mbalimbali zinanifanya nimudu gharama zote yakiwemo mahitaji yangu.
Mpaka Home: Unataka kutuambia huna mpenzi ambaye anakusapoti katika maisha yako?
Zuhura: Mpenzi yupo, lakini mahitaji yangu mengi huwa napambana mwenyewe.
Mpaka Home: Ukiwa na tatizo, nani wa kwanza kumkimbilia?
Zuhura: Huwa ni mama yangu mdogo ambaye anaishi maeneo ya Kariakoo kisha wanafuata ndugu zangu wengine.
Mpaka Home: Katika ishu zako zote, yaani kazi ya kupaka rangi, muziki, biashara na nyingine ipi inakuingiza mkwanja zaidi?
Zuhura: Hakuna zaidi ya kazi ya rangi, hata kama sijapata tenda sehemu huwa nakodisha mashine zangu na vifaa vingine vya ujenzi, jioni vinaleta hesabu.
Mpaka Home: Unapenda na kuchukia nini katika maisha yako?
Zuhura: Napenda maisha yenye furaha na amani, nachukia kunyanyasika.
Mpaka Home: Baadaye ungependa kuwa na familia ya watoto wangapi na umejiandaaje kwa hilo?
Zuhura: Ntafurahi zaidi nikifanikiwa kupata watoto wawili, nimejipanga na ninaendelea kujiandaa vyema ili baadaye watoto wangu waishi maisha mazuri.
Mpaka Home: Nini tofauti ya maisha yako ya zamani kabla hujawa maarufu na sasa?
Zuhura: Kwangu nadhani tofauti ni kujulikana tu, mambo mengine yako vile vile, huwa sina makuu.
Mpaka Home: Unauzungumziaje uchaguzi mkuu wa 2010 na sanaa yako ya muziki kwa ujumla?
Zuhura: Nawaasa Watanzania wachague viongozi watakaowaletea maendeleo ili baadaye wasije wakajuta. Kuhusu muziki hivi sasa nimeachia kazi mpya yenye jina la Napagawa, albamu inakuja
Mpaka Home: Tunashukuru kwa ushirikiano wako Zuhura.
Zuhura: Mi pia nashukuru, karibuni tena.

Read More......
Wednesday, August 25, 2010 Posted in | | 0 Comments »


Binafsi nilivutiwa na marafiki hawa, nikaona siyo mbaya nyinyi wadau pia muwaone

Read More......
Posted in | | 0 Comments »

Safari yangu sana ilikuwa ni kwa njia ya reli ya kati, nikajitupa ndani ya train japo kuna sehemu nilibadili na kupanda mabasi
...nilipofika Tabora mjini ilibidi nipate mapumziko ya muda katika hospitali moja baada ya kuhisi uchovu wa nguvu
...hatimaye safari iliendelea
Nashukuru Mungu nilifika salama
Hapa ndiyo kitaani kwetu, maeneo ya Mpanda Hotel
Kwa wale waliyopitia katika shule hii ya sekondari ntakuwa nimewakumbusha mbali sana
Hili ndiyo jengo la Mahakama yetu ya mwanzo lililopo pande za Makanyagio

Nasikitika sikuwa hewani kwa takribani wiki tatu, hivyo basi ninayo kila sababu ya kuomba radhi kwenu hasa kwa wale wadau wa blog yenu hii ya ukweli, ebwanadaah. Sababu kubwa ilikuwa ni likizo ya kikazi ambayo ilinifanya nisafiri kwa ajili ya kwenda kuwajulia hali ndugu na jamaa huko nyumbani kwetu Mpanda, kwenye Mkoa mpya wa Katavi. Nashukuru Mungu nimerudi salama, mambo yetu yaani ishu za ukweli zitaendelea kudondoka pande hizi kama kawa. TUKO PAMOJA.

Read More......
Sunday, August 22, 2010 Posted in | | 0 Comments »

Ebwanadah wiki hii, ambayo inapatikana ndani ya gazeti la Ijumaa Wikienda kunako safu ya Abby Cool & MC George Over The Weekend inashuka kitaani na orodha ya mademu waliowahi kulala kitanda kimoja na dogo anayetesa katika muziki wa R&B pande za Marekani hivi sasa, Justin Bieber.
Kinda huyo raia wa Canada, akiwa ndiyo kwanza anagonga miaka 16 ya kuishi duniani tangu alipozaliwa mwaka 1994, tayari ameshakula bata na vimwana wawili, Caitlin Beadles kuanzia mwaka 2007-2008 kabla ya kufunga pazia na Kristen Rodeheaver mwaka 2009 huku maelezo yakisema kwamba, bado wapo pamoja hadi hii leo.
Wengi wa mashabiki wake waliotoa comments zao, walisema kwamba, dogo ni cheche sana na kama kwa umri huo tayari ameshamiliki vimwana wawili, basi akifikisha miaka ishirini huenda idadi ikawa kubwa zaidi.

Read More......
Posted in | | 0 Comments »



Mkali wa Hip Hop Bongo, Kala Jeremah, ambaye ali-spend miezi kadhaa jijini Kampala Uganda akiwa na mchuchu aitwaye Jesca, amerejea nchini kimya kimya akiwa mikono mitupu, tofauti na matarajio ya wengi kuwa angekuja na mamsapu wake huyo.
Akiteta na ebwanadaah juzi, sosi wetu alisema: “Jamaa karejea, lakini yupo peke yake, wengi tuliamini angekuja na demu wake, lakini ndiyo hivyo, msela kashuka mwenyewe.”
Kala alipopigiwa simu ili kufafanua, alikuwa na haya ya kusema: “Yeah! Ni kweli sijaja na Jesca, lakini hiyo haimanaanishi kwamba tumeachana. She is still my love, nimeshindwa kuja naye kwa sababu uhusiano wetu haujawa plain kwa wazee wake, na mimi kama muungwana, sikuona busara kutoroka naye, ila kwa taarifa yako, ndoto yetu ni ndoa.”

Read More......
Posted in | | 0 Comments »


Sistaduu anayefanya vyema kwenye game ya muziki wa Kizazi Kipya, Zuhura Mrisho anadaiwa kuwa mgumu kinoma kung’oleka kimapenzi na maneno ya kitaa yanasema kwamba, ili umpate basi lazima upitie kwa sangoma kuweka mambo sawa kwanza.
Akipiga stori na ebwanadaah hii, Zuhura ambaye pia aliwahi kuiwakilisha Bongo kupitia Shindano la kumtafuta Kisura wa Afrika, Nokia Face Of Afrika 2006, alisema:
“Najaribu kuyaweka maisha yangu mbele kwanza, mambo mengine baadaye, sipendi mambo ya mapenzi, kwa sababu najua hayana future, napambana na life kwanza.”
Hata alipobanwa aeleze kwasasa yupo katika uhusiano na nani alitilia ngumu, akieleza kwamba hayo ni maisha yake binafsi na hapendi kuingiliwa ingawa msimamo wake ulibaki kuwa hana time kabisa na wanaume.
Pamoja na stori hiyo, hivi sasa Zuhura anasikika na mzigo mpya unaokwenda kwa jina la ‘Napagawa’ songi ambalo ndani yake lina mashairi ya kimapenzi, akiwa amepiga kolabo na Kindago wa TMK Majita.

Read More......
Posted in | | 0 Comments »

"Kwa mwaka huu A.Y alianza kunyakua Tuzo ya Chaguo la Teneez ya Kenya, Kili Awards ya Tanzania na Museke Awards ya Ghana. Mwaka huu ni moto chini, sidhani kama kuna artist wa Bongo aliyekuwa nominee kwa awards za nchi tofauti na kushinda tuzo...Sasa A.Y amechaguliwa katika fainali za Tuzo za Ufaransa zilizopewa jina la Redio France Internationale Discoveries Awards 2010 (Rfi Prix Decouvertes 2010) zitakazotolewa Septemba mwaka huu ndani ya Paris. A.Y anawaomba Watanzania wote kumpigia kura za kutosha ili aweze/tuweze kushinda tuzo hizo. Unaweza kupiga kura yako kupitia www.rfimusique.com. PAMOJA SANA".

Read More......
Posted in | | 0 Comments »





Mimi nilidhani Robot hutumika kufanyia kazi mblimbali hasa za nyumbani, kumbe hata kwenye uhusiano zinatumika!

Read More......
Posted in | | 0 Comments »

"Tunatarajia kufanya shoo ya nguvu maalum kwa vunja jungu Agosti 6 mwaka huu ndani ya Ukumbi wa Chuo cha Sanaa Bagamoyo. Ni Habari ndiyo hiyo A.Y na MwanaFA live ndani ya Bagamoyo," ni kauli kutoka kwa wakali hao wa Bongo Flava walipopiga stori na ebwanadaah.

Read More......
Sunday, August 1, 2010 Posted in | | 0 Comments »




Mwanadada hardcore kule pande za Obama, Trina ndiye anafunuliwa leo kuhusu mambo yake ya kimapenzi. EbwanaDaah.
Kwa mujibu wa site ya kiwanja ambayo imejipa jukumu la kufunua uhusiano wa kimapenzi wa mastaa mbalimbali, Trina siyo tu kwamba ameweka rekodi ya kufanya mapenzi na wanaume kadhaa, bali pia ametengeneza namba ya wanawake aliotenda nao usagaji.
C-Murder ndiye mwanaume anayetajwa wa kwanza kudondoka in bed na mgumu Trina kabla ya Jamie Foxx kuunga. Hata hivyo, kwa wote hao wawili, haitajwi ni lini alishirikiana nao kuibanjua amri ya sita.
Bilionea Sean Cutter ‘ Jay-Z’ au ukipenda muite Baba Beyonce, naye yumo kwenye orodha ya Trina ambapo mwanadada huyo alipopeana naye ‘shiti’, hakuona hatari kusagana na staa wa R&B, Kelly Rowland ambaye ni memba wa kundi marehemu la Destiny’s Child.
Baada ya Kelly, Trina alinogewa na mchezo wa usagaji, kwahiyo alipoondoka hapo, akaanza kupeana penzi la kisela na mwana Hip Hop wa kike mwenye sifa za kibabe, Missy Elliot.
Mark Wahlberg alimtumia Trina mwaka 2000 na Cash Money Brother, Lil Wayne alipumzika kwa mdada huyo kuanzia mwaka 2005 lakini ilipofika mwaka 2006, kila mtu alianza kivyake.
Rasi Baker aligusa mwaka 2007 na mwaka huo huo, Kenyon Martin alichangamsha naye damu.
Jina lake kamili ni Katrina Le`verne Taylor, umri wake ni miaka 31. Alizaliwa Desemba 3, 1978, Miami, Florida, Marekani. Dini yake ni Mkristo.

Read More......
Posted in | | 0 Comments »