ILI MUZIKI WETU UWEZE KWENDA KIMATAIFA NI LAZIMA TUBADILIKE, SAPOTI YAKO PIA MUHIMU

Mkubwa Fella na Bi. Cheka wakila pozi
Mi pia niliuza na Bi. Cheka
Bi. Cheka akiandaliwa na Producer Sulesh wa Poteza Rec, kabla hajaanza kurekodi

Kutoka ndani ya Familia ya Mkubwa na Wanawe, Bibi mwenye umri wa miaka 51 sasa yuko tayari kutoka na ngoma yake ya kwanza kupitia tasnia ya muziki wa kizazi kipya.
Anaitwa Bi. Cheka Hija ambaye alipiga stori na ebwanadaah na kuweka wazi kwamba, alikuwa anauzimia muziki tangu miaka ya 1970 lakini ndoto zake zimeanza kutimia mwaka huu mwanzoni alipokutana na Mkubwa Fella.
"Niko tayari kutambulisha ngoma yangu mpya ambayo nimefanya na Temba, nina uwezo wa kuimba na kuchana, pia huwa siandiki mistari kwenye makaratasi bali huwa natoa kichwani moja kwa moja,"alisema Bi. Cheka.

Tuesday, February 7, 2012 Posted in | | 0 Comments »

One Responses to "BIBI WA MIAKA 51 ANAGONGA BONGO FLAVA"

Write a comment