ILI MUZIKI WETU UWEZE KWENDA KIMATAIFA NI LAZIMA TUBADILIKE, SAPOTI YAKO PIA MUHIMU

Mimi na Bi Cheka
TMK Family
Bi Cheka studio

Kutoka ndani ya familia ya Mkubwa na Wanaye, sasa ni zamu ya Bi. Cheka kusimamishwa mbele ya jamii baada ya kazi yake kumtambulisha vyema na kuwafanya baadhi ya mashabiki wasiamini kama na umri wa miaka 51 kuelekea 52.
Ishu ni kwamba, Bibi huyu mwenye maskani yake pande za Bagamoyo, Pwani atatambulishwa kwa mara ya kwanza kwa mashabiki wa Morogoro siku ya Sikukuu ya Pasaka ikayoadhimishwa duniani kote Aprili 8, mwaka huu ndani ya Uwanja wa Jamhuri.
Meneja wake, Said Hassan Fella 'Mkubwa' amesema na Ebwanadaah leo kwamba,Bi. Cheka atapigwa tafu na kundi zima la TMK Wanaume Family, bila kuvisahau vichwa kibao vinavyounda Mkubwa na Wanaye kama Aslay, Dogo Mu, Easy Man na vingine kibao, huku wasanii waalikwa akiwemo Ferooz wakiungurumisha shoo za mwaka 2012. Ebwanaeeeee, Morogoro siku hiyo sogeeni pande za Jamhuri mshuhudia umri mkubwa, damu changa.

Wednesday, March 28, 2012 Posted in | | 0 Comments »

One Responses to "BI CHEKA KUTAMBULISHWA MORO PASAKA"

Write a comment